Wasemaji wa Kisekta
@actbarazakivuli
Official Account of the @actwazalendo Shadow Cabinet Research Office (SCaRO) under the office of the Party Leader @SemuDorothy and shadow PM @MchinjitaIR
ID: 1495511708860915714
http://www.actwazalendo.or.tz 20-02-2022 21:33:34
2,2K Tweet
2,2K Takipçi
189 Takip Edilen
"Mwaka 2021 Serikali imepora na kubadilisha ardhi ya vijiji kuwa ardhi ya hifadhi kwa kuanzisha hifadhi ya Igombe bila ridhaa ya wanavijiji kupitia Mikutano Mikuu ya vijiji." Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria Maharagande Mbarala #TaifaLaWote #MaslahiYaWote ACTWazalendo
"Tunataka Mkuu wa Wilaya ya Kaliua na Mkuu wa Mkoa wa Tabora wawajibishwe kwa ushirika wao wa kuruhusu vikosi vya Ulinzi JWTZ, wanamgambo na askari wa TFS kufanya uonevu kwa wananchi wa Vijiji vya ISAWIMA." Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria Maharagande Mbarala #TaifaLaWote
"Tunalitaka Bunge la Jamhuri ya Muunga ya Tanzania kuunda kamati ya uchunguzi wa matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu yaliyofanywa katika vijiji vya ISAWIMA huko Kaliua Mkoani Tabora." Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria Maharagande Mbarala #TaifaLaWote #MaslahiYaWote ACTWazalendo
"Rais Samia Suluhu aunde KAMATI ya kupitia maeneo yote yenye migogoro ya mipaka kati ya vijiji na mamlaka za hifadhi. Aidha hatua zichukuliwe kwa wote waliovunja haki za binadamu huko Kaliua kuanzia 2021 hadi sasa." Waziri Kivuli Katiba na Sheria wa ACTWazalendo Maharagande Mbarala
Ahsante kwa utumishi wako uliotukuka. ACTWazalendo #AhsanteBabuDuni #TaifaLaWote #MaslahiYaWote #ZanzibarMpya #ZanzibarMoja #MamlakaKamili
Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria wa ACTWazalendo, Ndugu Maharagande Mbarala anazungumza na waandishi wa habari muda huu. Tufuatilie youtube youtube.com/live/XPQ-p7CYP…
Waziri Kivuli wa Maji wa ACTWazalendo, Ndugu Sinta Cornely , anafanya ziara ya kusikiliza Wananchi juu ya kero za maji katika Mkoa wa Mara. #TaifaLaWote #MaslahiYaWote
"Hatuogopi kufikishwa mahakamani sakata la raia kuhamishwa kwa nguvu Kaliua." Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria Maharagande Mbarala #TaifaLaWote #MaslahiYaWote ACTWazalendo
RC TABORA ASITUTISHE, HATUOGOPI! RC Tabora Paul Chacha ametoa maneno ya kumtisha Msemaji wa ACT Wazalendo wa Sekta ya Katiba na Sheria Ndugu Maharagande Mbarala kuwa atamfikisha kwenye vyombo vya dola ahojiwe kutokana na kueleza ukweli kuhusu operesheni za kikatili zinazoendeshwa na
"Nyumba zimechomwa moto, shule zimevunjwa, mifugo imeuliwa, mazao yameporwa, na kumetokea matukio ya ubakaji na mauaji kwenye Operesheni za kikatili zinazoendeshwa na TAWA, TFS kwa kushirikiana na vyombo vya dola Kaliua." Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria Maharagande Mbarala
"ACTWazalendo imeguswa na kulaani vikali taarifa za kutekwa na kuuawa kwa aliyekuwa Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa Ndg. Ally Mohammed Kibao kinachohusisha vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi." Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani Dahlia Majid #HakiItendeke
"Kuwa mpinzani si dhambi, CCM iache kuteka Wapinzani." Waziri Kivuli wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Monalisandala #Miezi10 #WanachamaMilioni10 ACTWazalendo