Samia Suluhu
@SuluhuSamia
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. President of the United Republic of Tanzania
ID:2652554565
29-06-2014 07:42:17
1,2K Tweets
1,6M Followers
27 Following
On behalf of the Government and the people of The United Republic of Tanzania, I extend my heartfelt congratulations to the 57th Prime Minister of United Kingdom, Rishi Sunak I’m looking forward to taking our bilateral ties to greater heights. Karibu Tanzania.
Nawapongeza wanangu Ibrahim na Fadi (Ramadhan Brothers) kwa kipaji na ubunifu wenu wa kucheza sarakasi. Onesho lenu kupitia kipindi Australia's Got Talent limeitangaza vyema nchi yetu ya Tanzania na nawatakia kheri katika kuendeleza sanaa yenu na kushiriki katika maonesho mbalimbali.
Mmenifurahisha sana Watoto wangu SERENGETI GIRLS kwa kuandika historia ya kufuzu kuingia robo fainali ya Michuano ya Kombe la Dunia kwa Wanawake chini ya miaka 17 nchini India. Mmefanya jambo kubwa kwa nchi yetu Tanzania na nawatakia kheri katika hatua ya robo fainali.
Kongole Simba Sports Club kwa ushindi wa 1-0 (ushindi wa jumla 4-1) mlioupata dhidi ya timu ya Primeiro De Agosto ya Angola na hivyo kufanikiwa kuingia hatua ya makundi ya klabu bingwa Barani Afrika. Nawatakia kila kheri katika michuano inayofuata.
Hongereni Vijana wangu SERENGETI GIRLS kwa ushindi wa 2-1 mlioupata leo dhidi ya Ufaransa. Nawaomba Watanzania tuendelee kuwaombea na kuwatia hamasa vijana wetu ili waendelee kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania katika Kombe la Dunia kwa Wanawake chini ya miaka 17 huko India.
Nawatakia nyote kheri ya Sikukuu ya Maulid un-Nabi. Sherehe hii ya kukumbuka kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAW) iwe tafakari njema tunapoendelea kufanya kazi kuijenga nchi yetu na watu wake, na kuitunza amani, umoja na mshikamano tulio nao.
#MaulidNabiMuhammadSAW
Nimefurahi kushiriki sherehe za uapisho wa Rais wa 5 wa Kenya Mhe. William Samoei Ruto, PhD. Nampongeza Mhe. Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta kwa kumaliza uongozi wake na nawapongeza Wakenya wote kwa kukamilisha mchakato wa uchaguzi kwa amani. Tuendelee kushirikiana kuijenga Afrika Mashariki.
Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha Malkia Elizabeth II. Kwa niaba ya Watanzania wote, natuma salamu za pole kwa Familia ya Kifalme The Royal Family na raia wote wa Uingereza. Malkia atakumbukwa duniani kote kama nguzo ya Amani, Umoja na Utulivu.