WARAKA wa Serikali wa kuzuia na kuvunja Nyumba za Ibada waanza kazi. SERIKALI IMEVUNJA MSIKITI Chalinze.
Rais wetu Samia, Mwenyezi Mungu si CHADEMA, ACT, CUF nk.
Tunakushauri futa waraka huo, jenga Msikiti uliobomolewa na umtake msamaha Mola wako. Yeye ndiye aliyekupa Urais.
Utekwaji wa raia Tanzania unaongezeka: Trh 5/7/23 katekwa Aflah Nawanda (Dar). Trh 7/2/24 katekwa Imam Shaaban Khamisi (Magole Dar).
Trh 13/3/24 katekwa Imam Abdurahman (Geita).
Anayetekwa Tanzania maana yake kaondolewa duniani.
Ni kweli Serikali haiwajui wanaoteka raia?
Polisi TZ wamekiri kumshikilia Imamu Yasin. Pia wamekiri utekwaji raia upo ila wao hawahusiki na waliotekwa na kupotea kabisa.
Lakini utaratibu walioutumia kumchukua imamu ndio huo huo uliotumika kwa mamia ya raia waliopotea kabisa. Katika hali hii mtuhumiwa wa utekaji ni nani?
“Mwanangu hajaugua wamemuuwa”. “Mama Samia wewe ni mzazi, mtoto anauma”.
Hayo ni malalamiko ya mzazi ambaye mwanaye kafa mikononi mwa Polisi Karatu.
Msiba mkubwa Tanzania ni pale raia wanapolalamika uvunjwaji wa haki za msingi lakini viongozi hawajali wala kuzuwia matukio hayo.
Wagonjwa wa figo wanatozwa Sh. 400,000/600,000, kila juma katika hospitali za Serikali. Tungenunua magari ya kawaida, mapesa yatakayobaki yangenunua mashine za kutosha wagonjwa wakasafishwa figo bure kama Komoro. Si sawa kununua magari ya kifahari wakati hospitali hazina uwezo.
Toka 2013-2024, watu wanatekwa na kupotezwa. 2023, Shura ya Maimamu ilitoa ripoti ya uchunguzi. Katika ripoti hiyo jumla raia 236, wametekwa na kupotezwa. Kauli ya CCM “HAWA TUKIWAPOTEZA MSIWATAFUTE” inawafanya watuhumiwa Na.1. Kama taifa linajali uhai wa raia Dola ichukue hatua.
Si sahihi kutukanwa Raia au Kiongozi. Lakini mazingira yanaonesha CCM NDIO MWALIMU WA MATUSI KWA VIONGOZI. Moja ya ushahidi ni SAUTI YA KISONGE. Kwa miaka mingi imefurika matusi kwa Maalim Seif Sharif Hamad. Waandishi na Wahariri wa Kisonge hawajatekwa wala kupotezwa.
SALAMU: 1. Muungano haukupata ridhaa ya Wananchi. Si sawa kutoa kafara mataifa yetu kwa sababu ya Muungano wa Viongozi 2.
Inasemwa Kero zimekwisha, haziwezi kwisha bila makubaliano halali na Katiba ya Serikali 3. 3. Matokeo, miaka 60 sasa serikali zote 2 na raia ni maskini sana.
MAUWAJI ya kiholele yanakomaa nchini kwetu. Ni yale ya kutekwa na kupotezwa au kupatikana Maiti kwa utata. Watekaji huwa na Magari, Redio, Silaha pia hujitambulisha ni Usalama. Kwa hali hiyo Raia wanapo tuhumu, wazingatiwe badala ya kutishwa. Uhai ni kitu kibwa si cha kuchezewa.
KELELE ZA KUTEKWA RAIA TANZANIA ZINAONGEZEKA. Leo mke wa Abdallah Muna amesema: Mume wangu tarehe 31.1.24, (aliripoti Polisi Arusha)”. “Baada ya kutoka kuna watu walimfuatilia”. “Toka siku hiyo (ametekwa), hajapatikana tena”.
KAMA WANAOTEKWA NI WAHALIFU WAPELEKWE MAHAKAMANI.
MASHEIKH 7 WAMEHUKUMIWA LEO DAR. Saidi Bakari kahukumiwa kunyongwa. Abubakar Paulo-kunyongwa. Othman Khamis-miaka 20. Ahmed Musa-miaka 20. Musa Hasan- ameshinda. Hussein Ali - kashinda. Bakari Juma-kashinda. Wamekaa gerezani (2015-2024) miaka 9. Utawala wetu Dhulma juu ya dhulma.
MASHEIKH 4, WAMESHINDA KESI JANA, POLISI WANAWASHIKILIA. Ni: Ali Othman, Shaaban Bakari, Faraji Ali na Musa Mtweve. Tuhuma: Kufanya mazoezi ya kijeshi. Wamekaa gerezani miaka 11 (2013-2024). Wakubwa zungumzeni na vyombo vyenu vizingatie ubinadamu, viheshimu haki, uhuru na sheria.
Faida na hasara za Muungano kwa ZNZ na TNG, hasara ni kubwa mno kuliko faida. Na sasa mvutano unahatarisha Usalama wa Taifa. Ufumbuzi kila upande uitishe Kura ya Maoni Wananchi waulizwe: JE MNATAKA MUUNGANO? kama wanataka ok, kama hawataki kila nchi irudi katika SOVEREIGNTY YAKE.
Katika hafla ya WAKFU 13.05.24, Makamu wa Rais Dk. Mpango amewataka Maaskofu kupigania haki za Wananchi bila ya woga. Tunampongeza sana. Aidha kwa muktadha huo tunamkubusha kuombwa radhi Sheikh Farid na Sheikh Mselem kwa kuwekwa jela miaka 8 kwa kudai MAMLAKA KAMILI YA ZANZIBAR.
MASHEIKH 4, WAMESHINDA KESI LEO 4/6/24, MAHAKAMA KUU DAR. POLISI WAMEWACHUKUA.
Masheikh hao ni:
1. Zahaki Rashid.
2. Chande Rashid.
3. Jihadi Gaibon . Na
4. Rashid Omari .
Wamekaa jela miaka 9. Kwa zaidi ya miaka 8, upande wa serikali walishindwa kuleta ushadi Mahakani.
UTEKAJI NA MAUWAJI VINAZIDI TANZANIA. TUNAKUOMBA MH. RAIS ZUNGUMZA.
Juzi 6/9/24, Ali Mohd Kibao kachukuliwa na ‘Usalama’. Jana maiti yake imetupwa barabarani. Matukio haya yanazidi.
Utu, Uhai na Usalama wa Raia ni mambo muhimu kwa taifa makini. Sisi Tanzania tunaelekea wapi?
Tumesoma Rambirambi za Rais Samia kwa mauwaji ya kiongozi wa CHADEMA.
Lakini Raia ambao si wanasiasa, waliotekwa na kuuwawa ni wengi mno. Hawa nao vipi?
Mheshiniwa Rais Taifa linahitaji Tume ya Kijaji kuchunguza utekaji na mauwaji yote.
UTEKAJI: Jana nimetumiwa taarifa ya kutekwa Mwalimu wa Madrsa Saad Shaaban Mnubi.
Yeye alitekwa TRH 2/2/2023, saa 6 usiku nyumbani kwake Nyamanoro Mwanza. Watekaji walijitambulisha ni Usalama. Hili ni Janga lililoenea nchi nzima, tuungane kukemea na kushinikiza uchunguzi wa UN.